Kagame awasili na kupokelewa na Rais Magufuli

Rais wa Rwanda, Paul Kagame amewasili nchini leo Januari 14 kwa ziara ya siku moja na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais John Magufuli.

Baada ya kuwasili katika uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA), Rais Kagame alielekea katika chumba maalumu na kukaa hapo kwa takribani dakika 30.

Aliondoka uwanjani hapo saa 4:45 na kuelekea Ikulu ambapo atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli.

Hii ni mara ya pili kwa Kagame kuwasili nchini na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli tangu mwaka 2015. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2016 ambapo alifanya ziara na kushiriki maonesho ya 40 ya biashara (Sabasaba).


from MPEKUZI

Comments