Ujerumani: Marekani imeshindwa katika makabiliano yake na Iran

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Heiko Maas amekosoa sera za rais Donald Trump wa Marekani za kuongeza shinikizo dhidi ya Iran. 

Maas ameliambia gazeti la Ujerumani la Bild am Sonntag kwamba hawapaswi kudhania kwamba shinikizo kutoka nje dhidi ya Iran litaweza kuimarisha hali ilivyo nchini humo na kuongeza kuwa hatua kama hiyo ilikuwa na matokeo mabaya katika nchi kama Iraq. 

Maas amesema vitisho dhahiri pamoja na hatua za kijeshi na vitisho havijaweza kubadilisha tabia za kiuongozi za Tehran. 

Chama cha Social Democrat, SPD kimesisitiza kwamba mazungumzo ni njia muhimu itakayosaidia kupiga hatua na kuimarisha sera ya Ulaya kuelekea taifa hilo.


from MPEKUZI

Comments