CCM Yawaonya Walioanza Kampenzi za Urais na Ubunge Kabla Ya Wakati

Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amewaonya wanachama wa chama hicho tawala walioanza mikakati ya kutaka kupitishwa kuwania udiwani, ubunge na urais akibainisha kuwa kufanya hivyo ni makosa.

"Watu wa namna hiyo(walioanza mapema mikakati ya kutaka kupitishwa kuwania udiwani, ubunge na urais) hawatavumiliwa kwa kuwa taratibu za kuwania uongozi, nafasi mbalimbali katika chama hicho zipo wazi na zina muda wake" Dk. Bashiru Ally, Katibu mkuu wa CCM

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne Desemba 3, 2019 katika ziara yake kisiwani Pemba, Zanzibar wakati akizungumza na kamati ya siasa Wilaya ya Chakechake.


from MPEKUZI

Comments