Kiongozi wa Vyama 11 vya Siasa visivyokuwa na uwakilishi Bungeni, Abdul Mluya amesema hawawezi kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kama Vyama vingine kwasababu 'mwenye Njaa hawezi Kususia chakula'.
Vyama hivyo ni DP, SAU,NRA,ADC, UDP,UMD,CCK,TADEA, DEMOKRASIA MAKINI, TLP,AAFP.
Vimetangaza uamuzi huo leo Ijumaa Novemba 8, 2019 jijini Dar es Salaam siku moja baada ya Chadema na ACT Wazalenfo kujitoa kushiriki uchaguzi huo .
Vimesema vitashiriki vikiamini Wizara ya Tamisemi inayosimamia uchaguzi huo itatenda haki kwa kuwarejesha wagombea wake walioenguliwa kushiriki uchaguzi huo.
“Tunaamini watarudishwa kwa sababu wamekidhi matakwa. Tunataka tushindane kwa hoja na sera kwenye mikutano ya hadhara,” amesema katibu mkuu wa DP, Abdul Mluya kwa niaba ya viongozi wa vyama hivyo.
Vimetangaza uamuzi huo leo Ijumaa Novemba 8, 2019 jijini Dar es Salaam siku moja baada ya Chadema na ACT Wazalenfo kujitoa kushiriki uchaguzi huo .
Vimesema vitashiriki vikiamini Wizara ya Tamisemi inayosimamia uchaguzi huo itatenda haki kwa kuwarejesha wagombea wake walioenguliwa kushiriki uchaguzi huo.
“Tunaamini watarudishwa kwa sababu wamekidhi matakwa. Tunataka tushindane kwa hoja na sera kwenye mikutano ya hadhara,” amesema katibu mkuu wa DP, Abdul Mluya kwa niaba ya viongozi wa vyama hivyo.
from MPEKUZI
Comments
Post a Comment