CAG Kichere atambulishwa Bungeni

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere leo Jumatatu Novemba 11, 2019 ametambulishwa rasmi bungeni jijini Dodoma, ambapo Spika Job Ndugai ameahidi kuwa, bunge litampatia ushirikiano mkubwa. 

"Nataka nimuhakikishie kuwa, Bunge litakupa ushirikiano wa kila aina na wala hatuna tatizo na ofisi ya CAG kwa hiyo tutakuwa pamoja," amesema Ndugai.

Spika amesema leo mchana atakutana na CAG na wenyeviti wa kamati pamoja ili wajadiliane pamoja na kuzungumza baadhi ya mambo.


from MPEKUZI

Comments