Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Lakamata Silaha Mbili Aina Ya Short Gun.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limekamata silaha mbili aina ya Short Gun zikiwa na risasi mbili ambazo zilikuwa kwenye mtutu wa kila silaha ambazo zilikuwa zimefichwa kwenye mfuko wa plastiki.

Kufuatia msako mkali uliofanyika Oktoba 17, 2019 saa 17:00 jioni huko maeneo ya Pambogo, mtaa wa Isengo, Kata ya Iyela, Tarafa ya Iyunga, Jiji la Mbeya, Jeshi la Polisi Mkoani hapa lilikamata silaha hizo ambazo zimetengenezwa kienyeji na baada ya kuzikagua zilibainika kutokuwa na namba za usajili.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ametoa  rai kwa wananchi kutoa taarifa za mtu/watu au kikundi cha watu ambacho wanakitilia mashaka katika maeneo yao ili ufuatiliaji ufanyike. 

Aidha ametoa rai kwa mtu yeyote anayemiliki silaha kinyume cha sheria kusalimisha silaha hiyo mara moja kituo cha Polisi


from MPEKUZI

Comments