Zaidi Ya Vijana 500 Nchini Tanzania Wanatarajia Kukutana Jijini Dodoma Agosti 15 Katika Kongamano La Vijana

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Katika kuadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa ya  vijana Duniani ambapo  huadhimishwa Agosti 12 kila mwaka ambapo kwa Tanzania Maadhimisho hayo  kwa Mwaka 2019 yamesogezwa mbele hadi Agosti 15 na  16,2019  ,Zaidi ya vijana 500 kutoka Tanzania  wanatarajia kukutana jijini Dodoma .
 
Akizungumza na Waandishi Wa Habari leo Agosti ,14,2019 Jijini Dodoma ,Meneja  Mradi wa shirika la Kimataifa la  idadi ya Watu  [ UNFPA]  kwa Tanzania , katika kitengo cha Maendeleo ya vijana Dkt. Majaliwa Marwa amesema mwaka huu itakuwa ni kutimiza miaka 20 tangu maadhimisho hayo kuanzishwa maadhimisho hayo 
 
Ametaja Malengo ya Maadhimisho hayo kuwa ni pamoja na kupanua wigo uelewa juu ya vijana pamoja na changamoto zinazowakabili na Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kasim Majaliwa na mada zitakazowasilishwa ni pamoja na na elimu ya uzazi kwa vijana pamoja na changamoto za ajira kwa vijana.
 
Kwa Upande wake,Mwakilishi wa Shirika linaloratibu masuala ya vijana Tanzania[Restless Development] Bw.Ridhione Juma amesema  shirika hilo litahakikisha  kuwa na ulinganifu kwa makundi ya watu maalum ikiwa ni pamoja na watu wenye ulemavu huku katibu wa Asasi ya Vijana Tanzania [AFriYAN] akiishukuru Serikali ya Tanzania kwa Kutoa Elimu Bure.
 
Afisa  Mawasiliano  wa shirika la  Kazi Duniani [ILO]kwa Afrika Mashariki  Bw.Magnes Minja amesema utafiti uliofanyika mwaka 2014 ulibaini kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana ilikuwa asilimia 11.7&  ikilinganishwa na ukosefu wa asilimia 10.3 % kwa ukosefu wa ajira kiujumla huku meneja mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa[UN]Bi.Stella Vuzo akisema ajenda kuu ya Umoja wa Mataifa ni Malengo ya Maendeleo endelevu.
 
Naye  Mwakilishi wa UN Kitengo cha Habari nchini Tanzania ,Dokta.Warren Bright Hasheem amesema elimu inatakiwa kuwa jumuishi pamoja na ajira kwa vijana  pamoja na Malengo endelevu  ya miaka 15 na malengo ya millennia ya miaka 15.
 
Maadhimisho ya vijana Dunia yalianza yalianzishwa mwaka 1999 katika mkutano mkuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa ambapo kauli mbiu mwaka 2019 ni Elimu.


from MPEKUZI

Comments