VIDEO: Tazama Hapa Kangi Lugola Alivyojitosa Kucheza Mbele ya Rais Magufuli

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola  jana alishindwa kujizuia na kuamua kwenda kuungana na Bendi ya polisi nchini Tanzania  kusakata muziki na kuonyesha naye ni mjuzi wa kucheza hali iliyoibua shangwe kutoka kwa watu waliohudhuria shughuli hiyo.

Tukio hilo lilitokea jana  Jumatatu July 15 wakati wa  hafla ya ufunguzi wa nyumba 20 za polisi eneo la magogo mjini Geita.

Uzinduzi huo ulifanywa na Rais wa Tanzania, John Magufuli ambapo bendi hiyo ilionyesha uhodari wake wa upigaji mzuri wa tarumbeta uliombatana na mbwembwe za wapigaji ulikuwa kivutio kilichowafanya viongozi washindwe kuvumilia kukaa kwenye viti na kushuka kutoka jukwaa kuu na kwenda kuwatunza

==>>Tazama Video Hapo Chini


from MPEKUZI

Comments