Taarifa Mbalimbali Za Uhalifu Kutoka Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya

KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WANNE KWA TUHUMA ZA WIZI NA KUGHUSHI NYARAKA MBALIMBALI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wanne [04] ambao ni:-
1.     PILI OMARI [30] Mkazi wa Mbezi – Dar es Salaam
2.     HAMIS NGOWI [40] Mkazi wa Dar es salaama na
3.     OMARY MOHAMED [41] Mwalimu na Mkazi wa Nzovwe
4.     MARTHA KASMIRI [34] Mkazi wa Dar es salaam - Mbezi kwa tuhuma ya wizi katika Benki.

Mnamo tarehe 13.05.2019 saa 14:00 mchana huko katika Benki ya Posta tawi la Mwanjelwa iliyopo Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi kwa kushirikiana na maafisa wa benki hiyo waliwakamata PILI OMARI [30] na MARTHA KASMIRI [34] wote wakazi wa Dar es salaam - Mbezi wakiwa na nyaraka ‘salary slip’ zenye majina ya watu wengine ambao ni watumishi wa idara ya elimu, vitambulisho vya mpiga kura, fomu za utambulisho kutoka Jiji, fomu za mikopo kutoka benki ya Posta na barua za uthibitisho kutoka kwa mwajiri ambazo ni za kughushi.
Watuhumiwa wengine ambao ni HAMIS NGOWI [40] mfanyabiashara na mkazi wa Dar es salaama na OMARY MOHAMED [41] mwalimu na mkazi wa Nzovwe wamekamatwa wakati mtuhumiwa HAMIS NGOWI @ OPTATI NGOWI alipopekuliwa alikutwa na:-
1.     Mihuri 6 ya idara tofauti za serikali.
2.     Laini 10 za mitandao ya simu Vodacom, Tigo na Halotel,
3.     Picha ndogo 3 za watu tofauti ya jinsia ya kike,
4.     Funguo 2 za gari,
5.     Fomu za utambulisho kutoka Jiji,
6.     Fomu za mikopo kutoka benki ya Posta,
7.     ‘Salary slip’ pamoja na barua za uthibitisho kutoka kwa waajiri. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.
 
KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WAWILI WANAOJIHUSISHA NA MATUKIO YA UNYANG’ANYI, WIZI NA UBAKAJI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia vijana wawili ambao ni:-
1.     NASIBU JUMA [20] Mkazi wa Nzovwe Mbeya
2.     BRIGHT THOMAS [19] Mkazi wa Mtaa wa Ndanyella Mbeya
Kwa tuhuma ya kujihusisha na matukio ya unyang’anyi, wizi na ubakaji katika maeneo ya Nzovwe, Iyunga na Iwambi Jijini Mbeya.
Watuhumiwa walikamatwa mnamo tarehe 14/05/2019 huko Iyunga katika Klabu cha Pombe cha London kilichopo Jijini Mbeya na katika upekuzi watuhumiwa walikutwa na :-
1.     Mapanga mawili [02]
2.     Mizula miwili [02]
3.     Makoti meusi mawili [02]
Katika mahojiana na watuhumiwa wamekiri kuhusika katika matukio mbalimbali kama ifuatavyo:-
Mnamo tarehe 26/03/2019 saa 22:00 usiku huko Mtaa wa Inyala uliopo Kata ya Iyunga na Tarafa ya Iyunga ambapo walivamia nyumbani kwa Mwalimu wa Chuo MUST aitwaye WILLIAM MBATTA na kumjeruhi kwa mapanga sehemu ya kichwani na kisha kutoweka.
Mnamo tarehe 30/03/2019 saa 22:00 usiku katika viwanja vya MUST walimjeruhi ALLEN NYITTI kwa kumkata panga kichwani, kiunoni na tumboni na kupora simu aina ya Samsung Galaxy na pesa taslimu Shiling 21,000/=
Mnamo tarehe 05/04/2019 saa 02:00 usiku huko katika Mtaa wa Ndanyella, Kata ya Nzovwe, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya walimvamia FATUMA HAJI [21] walimbaka na kupora pesa taslimu shilingi 3,280,000/= pia waliiba TV aina ya LG na Redio Sub Woofer, Deck na simu ya mkononi aina ya Samsung J7. Mali zote zikiwa na thamani ya shilingi 4,120,000/=
Mnamo tarehe 04/05/2019 saa 02:45 usiku huko Kota za Tazara zilizopo Iyunga Mbeya walivamia nyumbani  kwa FRANK CHARLES na kumjeruhi kwa kumkata na mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake yeye na mke wake aitwaye VICTORIA SAMWEL pamoja na kupora TV aina ya Boss yenye ukubwa wa inchi 55.

KUKAMATA BIDHAA ZILIZOPIGWA MARUFUKU NCHINI.
Mnamo tarehe 16/05/2019 saa 05:00 Alfajiri huko maeneo ya Block “T”, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya, Askari Polisi wakiwa doria katika maeneo hayo waliliona gari lenye namba ya usajili T.937 CKD aina ya Toyota Mark II Blit na kulitilia mashaka na ndipo kukuta limebeba bidhaa mbalimbali zilizopigwa marufuku nchini ambazo:-
1.     Pombe kali aina ya PRINCE katoni sita @ chupa 20 sawa na chupa 120
2.     Pombe kali aina ya Officer”s Verve katoni 24 @ chupa 20 sawa na chupa 480
3.     Condom aina ya Ultimate Assured Protection katoni 63 ambazo zilitolewa na Serikali ya Marekani kwa nchi ya Zambia.
4.     Panga moja.
5.     Carolight 120ml pcs 36
6.     Citrolight 120ml pcs 84
7.     Coco Pulp 150mls pcs 24
8.     Coco Pulp 500mls pcs 06
9.     Coco Pulp 300mls pcs 36
10. Coco Pulp Lightening oil 50mls pcs 72
11. Coco Pulp 50g pcs 06
12. Carotone Crème ndogo 65mls pcs 24
13. Cocoderm pcs 06
14. Clinic Clear pcs 06
15. Extra Clair 120mls pcs 54
16. Elle 5 Crème pcs 3
17. Diproson tube 30g pcs 74
18. Diproson lotion 30mls pcs 48
19. Top Lemon Plus 170mls pcs 84
20. Carotone black spot corrector pcs 06
21. Dermotyl tube 15g pcs 10
22. Dermotyl lotion 30mls pcs 90
23. Dodo Crème ndogo pcs 06
24. Clairmen pcs 12
25. Bronz tone crème 125ml pcs 15
26. Miki Clair 160ml pcs 48
27. Movate Cream 30g pcs 50
28. Oranvate gel 30g pcs 50
29. Beaution Cream 330mls pcs 12
30. Miss Caroline 150mls pcs 12
31. Carolight Cream 120mls pcs 78
32. Diana lotion 30mls dozen 03 sawa na pcs 36
33. Teint Clair 150mls pcs 48
34. Betasol lotion 30mls pcs 36
35. Betasol tube 15g pcs 40
36. Perfect white cream 150mls pcs 12
37. Perfect white lotion 30mls pcs 06
38. Lemon vate cream 30g pcs 40
39. Mont Claire 30g pcs 10
40. Neoprosone Gel 30g pcs 10
41. Epiderm Creme 15g pcs 41
42. Epiderm Crème 30g pcs 24
Gari hilo lilikuwa likitokea Tunduma kuja Mbeya likiwa na bidhaa hizo. Gari pamoja na vielelezo vipo kituo cha Polisi. Msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa waliokuwa wakisafirisha bidhaa hizo unaendelea.

KUPATIKANA NA POMBE KALI ZILIZOPIGWA MARUFUKU NCHINI.
Mnamo tarehe 13.05.2019 majira ya saa 21:00 usiku huko maeneo ya Iwambi, Kata ya Iwambi, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya. Polisi walimkamata kijana mmoja aitwaye ELIA MWAKALIKWE [25] Mkazi wa Iwambi akiwa na Pombe Kali zilizopigwa marufuku nchini aina ya Verve katoni 27 zikitokea nchini Zambia.

Imetolewa na;
[ULRICH O. MATEI – SACP]
   KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


from MPEKUZI

Comments