Rais Magufuli Awatumbua Wakurugenzi Wawili

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbozi mkoani Songwe Bw. Adelius Kazimbaya Makwega na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui mkoani Tabora Bi. Hadija Makuwani.

Mh Rais ametangaza uamuzi huo katika kikao cha kazi kati yake na Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala za Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala za Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya kilichofanyika  leo Ikulu Dar es Salaam.



from MPEKUZI

Comments