Mchungaji Msigwa ahoji uhalali wa Spika Ndugai kumsimamisha Kuwasimamisha Uwakilishi wabunge wanaochaguliwa na Bunge kuwawakilisha katika mabunge mbalimbali

Mbunge wa Iringa Mjini, Mch. Peter Msigwa amehoji bungeni uhalali wa uamuzi wa Spika Job Ndugai kusimamisha uwakilishi wa Mbunge wa Shinyanga Mjini, Stephen Masele (CCM) katika Bunge la Afrika (PAP), bila Bunge la Tanzania kujadili

Jana Spika Job Ndugai alisema kuwa amemuandikia barua Rais wa PAP ya kusitisha uwakilishi wa Stehen Masele hadi Kamati ya Maadili itakapokamilisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake.
 

"Katika uwakilishi wa Bunge la Afrika kumetokea matatizo makubwa hasa kwa Mhe.Steven Masele matatizo ya kinidhamu,Tumelazimika kumrudisha nyumbani kuanzia Jumatatu, badala yake amekuwa akionyesha kugoma, ni kiongozi ambaye anafanya mambo ya hovyo hovyo". Alisema Ndugai.

“Uhalali unatoka wapi na hawa hawakuteuliwa wamechaguliwa na nilitaka kujua anasimamishwa na kiti bila kujadili inatuchafua kama Taifa. Bunge litakuwa na nguvu gani ya kuwalinda hawa tunaowachagua,” amehoji Mchungaji Msigwa.

Akijibu mwongozo huo, Chenge amemtaka Mchungaji Msigwa kutowahisha hoja kwa maelezo kuwa tayari jana Alhamisi, Spika Job Ndugai alilitolea uamuzi kwa kuomba wabunge wasubiri taarifa itakapowasilishwa bungeni watakuwa na nafasi ya kujadili kwani milango haijafungwa.


from MPEKUZI

Comments