Drake Kununua kava la simu yake kwa milioni 900

Rapa Drake si mgeni katika kupenda kumiliki vitu vya fedha kubwa, lakini hii imechukua vichwa vya habari zaidi kutokana na maamuzi alioamua kuyafanya. 

Mara nyingi haishangazi ukisikia Drake amenunua ndinga jipya kwa gharama lakini saivi ameripotiwa kununua kava la simu yake kwa gharama kubwa.

Drake ameripotiwa na mitandao mbalimbali nchini Marekani kuwa ameweka oda ya kutengenezewa kava maalumu la Iphone yake yenye madini ya almasi. 

Kava hiyo maalumu aliyoweka oda Drake itakuwa na nakshinakshi za madini ya dhahabu nyeupe na blue ya gramu 18 ambazo ni dola 400,000 ambazo ni zaidi ya Sh milioni 900.

Staa huyo wa ngoma inayotamba ya ‘God’s Plan’, ameweka oda hiyo kwa moja katika ya sonara maarufu duniani wa masuala ya uuzaji vito vya thamani anayejulikana kwa jina la Jason Of Beverley Hills.

Waandishi wa Marekani wanadai kuwa Drake ambaye anapenda vitu vipya ikiwemo simu kila inapotoka atapata hasara kama kampuni ya Apple itatoa toleo jipya la simu ambalo huwezi kutumia kava lake la zamani.


from MPEKUZI

Comments