Wagonjwa MOI Kufanyiwa Upasuaji Bila Nusu Kaputi

Na Andrew Chale
TAASISI ya tiba ya Mifupa MOI imeanzisha huduma ya kutoa dawa za usingizi (Reginal block Anaesthesia) ambapo eneo husika linalofanyiwa upasuaji ndilo litakolo husika kwa kuzuia mishipa ya fahamu na hivyo mgonjwa kuwa macho na kuzungumza au hata kusoma gazeti

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface katika hafla ya kuwapokea wakufunzi wawili kutoka Chuo kikuu cha Latvia cha nchini Latvia ambao watatoa mafunzo hayo ya kibingwa ya kuzuia mishipa ya fahamu katika eneo linalofanyiwa upasuaji badala ya kumlaza mgonjwa usingizi (Nusu kaputi) kwa zaidi ya siku kumi kwa madaktari bingwa wa MOI na madaktari walio mafunzoni

“Huu ni muendelezo wa mafunzo ambayo tulishayaanzisha kwa mdakatari wetu , lengo kubwa la mafunzo haya na ujio wa wakufunzi hawa ni kuhakikisha huduma hii inaendlea kutolewa hapa MOI. Ni mbinu bora na salama ya kumlaza mgonjwa kwaajili ya upasuaji ambapo mgonjwa anaweza kufanyiwa upasuaji huku anasoma kitabu (Novel) ambapo baada ya upasuaji mgonjwa hapati maumivu makali na anaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani siku hiyohiyo” Alisema Dkt Boniface

Dkt Boniface amesema pamoja na wakufunzi hawa kutoa mafunzo , Taasisi ya MOI itasiani mkataba wa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Latvia lengo kuu ikiwa ni kubadilishana uzoefu katika utoaji wa huduma za kibingwa za Usingizi (Anaesthesia)

“Kwa kuanza tutasaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu ambapo watalaamu kutoka hapa watapata fursa ya kujifunza kwenye Chuo chao lakini pia watakuja hapa kutoa mafunzo ya muda mfupi kama ambavyo hawa wamekuja” Alisema Dkt Boniface

Dkt Boniface ameongeza kwamba kwa sasa Taasisi ya MOI imeanzisha huduma ya kulazwa na kufanyiwa upasuaji siku hiyohiyo yaani (Same day Surgery) hivyo huduma hii itatumika katika wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji na kuruhusiwa kwani wagonjwa hawapati maumivu makali baada ya upasuaji na hakuna masharti magumu baada kufanyiwa upasuaji

Kwa upande wake Profesa Alex Miscuks kutoka Chuo Kikuu cha Latvia amesema ni heshma kubwa kupata fursa ya kuja kubadilishana uzoefu hapa Tanzania kwani pamoja na kutoa mafunzo atapata fursa ya kujifunza mambo mengi.

“Nashukuru sana kwa kunialika, nimefurahi kukutana na madaktari wazuri na wazoefu hapa MOI, naamimi mimi pia nitajifunza mambo mengi kwenu, ahsnteni sana” alisema Prof Miscuks

Kwa upande wake Dkt Iveta Gobovska ambaye pia ni Mkuu wa kitengo cha wagonja mahututi katika hospitali ya Chuo Kikuu cha Latvia amesema amefarijika kupata fursa ya kuja kubadilishana uzoefu na madaktari wa Tanzania na anamini pande zote mbili zitanufaika na mafunzo haya.


from MPEKUZI

Comments