RC Makonda Awahimiza Wananchi Kujiunga Na Rais Magufuli Kuipokea Ndege Ya Sita Ya Serikali Airbus A220-300 LEO Mchana

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda anawaalika Wananchi wote Wapenda maendeleo kujiunga na Mtekelezaji namba moja wa Ahadi Rais Dkt. John Magufuli kwenye mapokezi ya Ndege ya Sita ya Serikali (Airbus A220-300) itakayowasili Nchini leo January 11 Saa sita Mchana ikitokea Nchini Canada.

Hafla ya mapokezi itafanyika kwenye Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere.

Rais Magufuli aliahidi na sasa anatekeleza

WANANCHI WOTE MNAKARIBISHWA


from MPEKUZI

Comments