BREAKING: Rais Magufuli Afanya Mabadiliko Baraza la Mawaziri....Afungua Ubalozi Mpya Nchini Cuba

Rais Magufuli leo amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri ambapo amemteua Angela Kairuki kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu/Uwekezaji.

Naibu Waziri wa Madini Dotto Biteko amekuwa waziri kamili wa madini, na Stanslaus Nyongo ataendelea kuwa maibu waziri wa wizara hiyo
 
Rais amemteua Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dr. Mpoki Ulisubisya kuwa balozi, kituo chake cha kazi kitatangazwa baadaye, pia Magufuli ametangaza kufungua ubalozi wa Tanzania nchini Cuba ambapo balozi atatangazwa baadaye.


from MPEKUZI

Comments