Askofu Zakary Kakobe Ammwagia SIFA Rais Magufuli Ujio wa Ndege Mpya

Askofu Mkuu wa kanisa la Full Gospel Bible fellowship (FGBF), Zakary Kakobe, ameweka wazi kukoshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli kwa kuweza kuingiza ndege nyingine ya Air Bus 220-300.

Askofu Kakobe ameyasema hayo leo katika mapokezi ya ndege ya sita zilizoingizwa nchini katika awamu ya uongozi wa Rais Magufuli.

Kakobe ametumia nafasi yake ya kuliombea taifa kutoa maneno hayo. 

“Mheshimiwa Rais mimi huwa ni mbishi kidogo na ukiniona nimekanyaga mahali kama hapa ujue umenikosha na sijui kama kuna watu wengine wamekoshwa kama Kakobe kwa ajili ya haya yanayotendeka,” amesema Askofu Kakobe huku akishangiliwa na umati wa watu waliojitokeza

“Na wengine wanasema mnamwabudu na kumsifu wakati hata Biblia inasema anayestahili heshima apewe heshima, hivyo unastahili zote.”

Askofu Kakobe amesema suala la kuwakusanya watu wote bila kujali itikadi huo ndio uzalendo unaotakiwa.

Amesema, “Ukiona hizi shangwe na vigelegele japo sio wote wanaokusifu ujue kuna watu wanashangilia kazi zako na leo tunakusihi ujipongeze, ulale na ujue wapo watu wanakushangilia kwa kazi zako.”


from MPEKUZI

Comments