Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 32

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  

“Acha unafki mtoto wa kike. Umenionyesha  dhairi kwamba wewe sio mwanamke wa kuoa. Umenibagua kirangi na kuniiita sokwe. Sawa mimi ni sokwe, nakuomba usinipende na usokwe wangu. Nitatafuta sokwe mwazangu, niishi naye na nitavumiliana naye kwenye shida na raha, tabu na majanga kama uliyo nifanyia leo. TOKA NYUMBANI KWETU”
Nilizungumza kwa kufoka sana hadi mishima ya damua ikavimba katika mikono yangu. Camila taratibu akasimama na akaanza kunifwata kwa hatua za taratibu, jambo lililo nifanya niamke kiatandani na kumfwata sehemu nilipo, ili nimrudishe mlangoni n aondoke zake. Kitendo cha kumshika mkono wake, akachomoa  kisu cha kukunjua ndani ya kipochi chake.  Akanichoma kisu cha tumboni mwangu, jambo lililo nifanya nihisi maumivu makali sana ambayo toka kuzaliwa kwangu sikuwahi kuyapata.
 
“Ni bora tufe wote kuliko kuendelea kukukosa wewe”
Camila mara baara ya kuzungumza maneno hayo, akakichomoa kisu hicho kwa nguvu tumboni mwangu kisha naye akajichoma tumboni mwake na akawa wa kwanza kuanguka chini huku nami nikianguka pembeni yake.

ENDELEA                   
Camila taratibu akaanza kuuleta mkono wangu kwangu huku machozi yakiwa yanamwagika usoni mwake. Taratibu giza zito likaanza kunitawala usoni mwangu, kabla sijaipoteza nuru ya macho yangu. Nikamuona Ethan akisimama mbele yangu huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana. Ethana akatuwekea mikono yake kwenye majeraha yetu ambayoa baada ya sekunde chache, maumivu makali amnbayo tulikuwa tunayahisi, yakapotea na Camila akawa mtu wa kwanza kukaa kitako huku akijishangaa.
 
“Kwa nini umefanya hivi binti?”
Ethan alimuuliza Camila kwa sauti nzito sana hadi Camila akaanza kutetemeka.
“Nipo mbinguni ehee…..!!?”
Camila aliuliza swali ambalo lilizidi kumkasirisha Ethan, kwani alishika kwa mikono yake na kurushia kitandani na kutaka kumuadhibu.
“Ethan usifanye hivyo, nitalishuhulikia”
NIlizungumza huku nikijinanyua kitandani taratibu, Ethan akanitazama kwa macho yaliyo jaa hasira, kwa ishara ya kutingisha kichwa nikamuomba tena asiweze kufanya jambo lolote baya. Ethan akapotea ndani humu, taratibu nikasimama na kuanza kumfwata Camila kitandani alipo lala huku akiwa amejionea mauza uza.
“Ethan tupo mbinguni, etii?”
“Umeona wapi mbinguni kukiwa na vitanda, acha upuuzi Camila”
 
Nilizungumza kwa kufoka kidogo huku nikimtazama Camila usoni mwake.
“Kwa nini unakuwa mjinga, umeona kuniua ndio suluhisho la tatizo”
“Bila wewe Ethan tambua siwez…………”
Nikamzaba Camila kofi la shavuni mwake, ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kumpiga toka tuanze mahusiano. Camila akaa kimya huku akitazama chini na machozi yakimbubujika.
“Unakuwa mpumbavu, unakuwa mjingia, wewe ni mwanamke wa aina gani usiye elewa kwamba kuna maisha na kufa. Kuna kitu gani kimeingia kwenye ubongo wako. Au huko Tanzania walikuroga si ndio?”
 
Nilizungumza kwa kufoka sana hadi Camila akaanza kutetemeka, taratibu akanitazama huku nikishuhudia jinsi vidole vyangu vilivyo acha alama shavuni mwake.
“Nilikupenda, nilikujali na nikakueleza vitu vyangu vingi kwa ajili yako. Leo hii unataka kuniua nikiwa bado mdogo ili iweje eheeee”
 
Nilizungumza huku nikimtingisha Camila mwili wake. Camila kwa haraka akanishiaka mashavu yangu na kuanza ku.. midomo yangu, nikajaribu kumtoa, ila akaendelea kuning’ang’ania kwa nguvu sana. Kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivyo jinsi Camila alivyo zidi kuipoteza hasira yangu hadi mwishowe nikajikuta nikilainika na kuendelea kumN.. midomo yake.
Kweli mapenzi  yana nguvu sana kwenye mioyo ya watu wengi. Ndani ya muda mchache tu, tumejikuta tukisahau kila kitu ambacho kilitokea. Tukaanza kuvuana nguo zetu na ndani ya muda mchache tukajikuta tukiwa tupo kama tulivyo zaliwa.
Tukaanza kupeana burudani
“Nataka tena mume wangu”
“Ngoja kidogo nivute pumzi”

“Camila”       
“Mmmm…..”       
“Nani kakufundisha mambo haya?”
“Ohoo Tanzania hiyo mume wangu”
“Tanzania?”
“Eheee?”
“Ndio imekufundisha?”
“Yaaa….kun…a….aiiiss….ohooo….dada….”
“Dada mmoja alikuwa akitumfundisha maswala ya chumbani na hapa ndio ninafanya kwa vitendo”
“Mmmm….”
“Niamini mume wangu”
Camila hakutaka hata kunipa nafasi ya mashambulizi, alicho fanya ni kuzidisha kasi ya kiuno chake hadi nikajikuta waarabu wangu wakishindwa kujizuia na kutoka bila idhini yangu.
“Ohooo….ahaaaa”   
Camila alitoa miguno hiyo kisha taratibu akanilalia kifuani mwangu na kuanza kuninyonya midomo yangu taratibu kwa hisia kali sana. Katika mapenzi yetu toka nimfahamu Camila, leo hii ndio nimeweza kufurahia penzi lake kwa asilimia mia moja.
“Hii ni mbinu namba moja tu mume wangu tuliyo fundishwa. Kuna mbinu nyingine tisa bado sijazitumia”
 
“TISAAAAA…..!!!?”
“Ndio mume wangu”
“Ohoo Mungu wangu, utaniua mke wangu, si kwa utamu huu”
“Haa, sasa ulipo kuwa unataka kuniacha ulidhani kwamba mautamu haya ningempa nani jamani?”
Camila alizungumza kwa sauti ya kudeka hadi mimi mwenyewe nikabaki nikiwa na kigugumizi kizito.
“Leo sihitaji kurudi nyumbani, nata tupeane usiku kuacha na kama mama jisni alivyo sema, lazima unipatie mtoto”
“Ila kumbuka kwamba bado tupo shuleni?”
“Hivi kwa hili lililo jitokeza unahisi nitarudi tena shule. Siwezi kurudi shule, kwa sasa nataka kusimamia kampuni za baba yangu, mara baada ya kushinda kiti cha uraisi”
“Ohoo tena nimekumbuka kitu”
 
“Kitu gani?”
“Ngoja ninakuja”
Nilizungumza huku nikishuka kitandani, nikafungua kabati langu la nguo. Nikachukua tisheti pamoja na pensi fupi kiasi.
“Ethan unakwenda wapi?”
“Ninakuja sasa hivi mke wangu”
Nilizungumza huku nikivaa nguo hizi, nikatoka chumbani humu na kumuacha Camila kitandani. Nikampita bibi Jane Klopp sebleni pasipo kumsemesha chochote, nikaelekea kwenye jengo la ofisi, nikamkuta mwana sheria akiwa anazungumza na simu. Nikaka kwenye kiti changu na ofisini humu na nikamsubiria amalize kuzungumza.
“Mkuu nimesha weka taratiu zote za kutoa asilimia thelathini tulizo weka kwenye kampeni za mgombea uraisi ninasubiria tamko lako la mwisho tu nipitishe”
Mwanasheria alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Umesema umesha andaa jinsi ya kuzitoa asilimia zangu?”
“Ndio”
 
“Hembu ongeza asilimia ishirini na ziwe hamsini?”
“NIONGEZEE……!!??”
Mwanasheria aliniuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana, kwani maamuzi aliyo kuwa akiyategemea kutoka kwangu yamekuwa ni tofauti.
“Fanya kama nilivyo kuambia. Nina mipango mikubwa ambayo nimeifikiria, akikosa uraisi, mambo ninayo yafikiria nina imani kwamba hayato weza kwenda sawa”
Mwanasheria akajawa na kigugumizi kikubwa sana ambacho hakika kinaonyesha dhairi kumuweka njia panda.
“Piga simu na waambie kwamba Ethan Klopp ameongeza asilimia za kumdhamini mgombea uraisi na kama watahitaji kampeni yangu kubwa kwake, basi nitampatia”
“Kuna kitu gani kinacho endelea mkuu?”
“Nitakueleza. Niakwenda kulala sasa hivi, ukimaliza unaweza kwenda tu nyumbani sawa”
 
“ETHAN, ninakufahamu, hembu zungumza ni kitu gani kinacho endelea”
“Mimi na Camila tumesha rudiana”
“Nini!!!?”
Mwanasheria alizungumza kwa mshangao mkubwa sana.
“Ndio tumerudiana na sasa hivi huko ndani tunatafuta mtoto kufuta matatizo yetu. Hichi ninacho kifanya, ninawekeza kwa mwanangu na sio kwao umenielewa”
Mwanasheria akabaki akitabasamu, nikaanza kutembea hadi mlangoni mwa ofisi hii, kisha nikamgeukia.
“Iwe siri yako, mambo yanayo endelea kwenye mitandao ya kijamii, wewe yapotezee sawa”
“Sawa mkuu”
Nikatoka humu ndani na kuanza kuelekea ndani huku nikiwa nimejawa na furaha huku kichwani mwangu, nikiwa nawazia mbinu tisa zilizo bakia kwa Camila, kwani kama ni mbinu ya kwanza imenipagawisha namna hii, nina imani kwamba mbinu hizo tisa, zitanifanya niwe zuzu kabisa.
 
Nikamkuta dada Mery na mama wakiwa wamekaa sebleni, huku Mery akionekana kuwa na furaha kubwa sana na mazungumzo ambayo walikuwa wakizungumza na mama waliyakatisha mara baada ya kuniona.
“Nini?”
Dada Mery aliniuliza mara baada ya kuona nimemkazia macho sana.
“Hamna jamani”
“Mbona una cheka cheka?”
“Hata wewe mbona una cheka cheka. Hembu nenda ndani huko kuna mambo nahitaji kuzungumza na mama”
Nikatabasamu tu kisha nikaanza kupandisha ngazi, nilipo fika katkati ya ngazi, nikasimama kisha, nikanyata na kutega siko langu ili niweze kumsikiliza dada Mery ni kitu gani ambacho anakizungumza na mama.
“Yaani huwezi kuamini mama. Toka ulivyo nizaa na nijitambue kwenye mambo ya mapenzi, leo hii ndio nimekojo*** katika tendo la ndoa”
 
Nikajikuta nikitabasamu, na nikaendelea na mambo yangu huku nikijisemea kimoyo moyo kwamba Ethan amefanya yake. Nikaingia chumani na kumkuta Camila akiwa amejifunga shanga kiunoni.
“Za nini tena hizo?”
“Hii ni mbinu namba mbili mpenzi wangu”
Camila alizungumza huku akinishika mkono kuelekea kitandani, kabla hatujafika kitandani, akainama  jambo lililo sababisha hisia zangu kurudi kwa kasi sana.
“Nakupenda sana mume wangu”
“Nakupenda pia”
Simu ya Camila ikaanza kuita, akashuka kitandani taratibu, akaokota kipochi chake chini na kuitoa.
“Ni nani?”
“Baba”
“Ahaaa sawa”
“Ndio baba”
“Kweli?”
 
“Ohooo asante sana mume wangu”
Camila alizungumza kwa furaha huku akinikimbilia akanikumbatia kwa nguvu sana hapa kitandani nilipo lala.
“Huyu hapa zungumza naye”
Camila akaniwekea simu hii sikioni mwangu na nikaisikia sauti ya baba yake.
“Ndio baba”
“Nashukuru sana kwa kiwango ulicho kiongeza kwenye kampenzi zangu. Mungu azidi kukubariki”
“Nashukuru sana”
“Naomba pia unisamehe kwa yale yote yaliyo pita kwani ni tatizo letu”
“Nashukuru pia baba, tupo pamoja”
“Asante, haya endeleni kufurahia muda wenu”
“Nashukuru”
 
Nikamabidhi Camila simu yake.
“Ndio baba”
“Sawa, tutaonana kesho”
“Nakupenda pia baba”
 Camila akakata simu huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.
“Baba amefurahi sana kwa kuongeza asilimia zako kwenye kampeni zake za uchaguzi”
“Usijali, na ninawazo nimelipata”
“Wazo gani mume wangu?”
“Nahitaji kufanya matangazo ya kampeni yake. Umaarufu unaweza kumsaidia kuzidi kupata wafuasi wanao muamini”
Camila akanikumbatia kwa nguvu sana huku akiwa amejawa na furaha.
“Ndio maana ninakupenda sana Ethan wangu, nakuahidi sinto fanya ujinga wa aina yoyote kwenye mapenzi yetu”
“Usijali mke wangu, yaliyo pita acha yapite, ila kwa sasa tutazame haya yaliyopo mbele yetu”
 
“Nashukuru na ninafuraha kusikia hilo”
Taratibu tukakumbatiana na Camila huku nyuso zetu zikiwa zimejawa na furaha. Tukaingia bafuni na kuoga kwa pamoja kisha Camila akavaa nguo zangu za michezo na tukatoka sebleni. Bi Jane Klopp alipo tuona, usoni mwake akajawa na furaha kubwa sana.
“Atakuwa wa kike”
“Nani?”
Niliuliza huku nikitabasamu.
“Huyo muliye mtafuta”
“Jamani mama”
“Kweli vile atakuwa wa kike”
Bibi Jane alizungumza katika hali ya utani. Dada Mery naye akaja sebleni hapa na furaha ikaendelea kutawala katikati yetu. Dada Mery na Camila wakaandaa chakula cha usiku. Muda ulipo wadia wa chakula tukala pamoja na nikasaidiana na Camila kumrudisha mama chumbani kwake.
 
“Ethan”
“Naam mama”
“Usije ukamuacha huyu binti. Mukiendelea kuwa pamoja mambo yenu mengi yatafanikiwa. Camila, natambua una hasira za karibu na unajiamini sana, hembu jaribu kidogo kuzizuia hata kama kuna jambo kubwa limetokea katikati yenu. Hakika mutadumu kwa miaka mingi sana”
Bibi Jane Klopp alizungumza huku akiwa ametushika mikono yetu.
“Nashukuru sana mama na nitafanya hivyo”
“Sawa, naweza kulala sasa”
Nikambusu bibi Jane Klopp kwenye paji lake la uso kisha tukatoka ndani humu. Usiku mzima tuliutumia katika kuburudishana kwa kila aina ya kimapenzi. Asubuhi na mapema, kama kawaida yangu nikaanza kufanya mazoezi mepesi mepesi ili kuendelea kuuweka mwili wangu sawa. Jioni ya siku ya leo nikarudi kambini hukun ikiwa nimeongozana na Camila ambaye kwa sasa ahitaji hata niwe mbali naye. Wachezaji wezangu wakazidi kufurahi mara baada ya kuniona nimerudi nikiwa na afya njema. 
 
“Mwanangu shavu limekuwa, au ndio maisha mazuri?”
Frendando aliniuliza huku akiwa amejawa na furaha usoni mwake.Tukakumbatiana kwa muda kidogo.
“Ni shemaji yako ndio msababishaji wa haya yote”
“Samahani Ethan”
Muhudu wa hoteli hii tuliyo fikia, alizunumza huku akiwa amesimama pembeni yetu.
“Bila samahani”
 
“Kuna mzee pale anakuita”
Nikageuka nyuma yangu na kumuona mzee mwenye asili ya Kichina akiniita.
“Sawa”
Nilimjibu muhudumu huyu, kisha nikaanza kutembea hadi kwa mzee huyu, nikamsalimia kwa heshima zote kwa maana sifahamu ni nani.
“Ninaitwa Mr Shing Jing, nimetokea China”
“Nashukuru kufahamu”
“Kuna jambo kidogo nataka kushirikiana nawe, kama hoto jali naomba nafasi nikuonyeshe”
“Bila samahani”
Mzee huyu akachukua brufcase yake iliyopo pembezoni mwa miguu yake. Akaiweka mezani na kuifungua, akatoa bahasha ya kaki kubwa kiasi na kunikabidhi. Akaifunga brufcase yake na kuirudisha chini.
“Unaweza kufungua tu hiyo bahasha”
Nikaifungua bahasha hii, nikakuta picha nne ndani ya bahasha hii, nikaanza kutoa moja baada ya nyingine. Picha hizi zinamuonyesha mwana mama wa kiafrika akiwa amefungwa mikonono yake pamoja na mdomo wake na pembeni yake kuna wanaume wawuli walio shika mitutu ya bunduki.
 
“Hizi picha za nini kwangu?”
Mzee huyu akatabasamu huku akinitazama usoni mwangu.
“Huyo ni mama YAKO MZAZI, ana siku ya tatu toka vijana wangu wamshikilie. Biashara iliyopo hapa ni ndogo sana. Boksi jeusi, kwa uhai wa mama yako mzazi”
Maneno ya mzee huyu yakanitusha sana, nikazitazama picha hizi kwa umakini sana, taratibu taswira ya sura yangu nikaanza kuiona kwa mwanamama huyu jambo lililo nifanya nistuke huku mwili wangu ukisisimka hadi vinyweleo vyangu vya mwili vikaanza kunisiamama kwa mstuko huu nilio upata.

==>>ITAENDELEA KESHO


from MPEKUZI

Comments