Alichokisema Lulu Michael Kwa Mara ya Kwanza Tangu Amalize Kifungo Chake

Mwigizaji Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, amefunguka kwa mara ya kwanza tangu alipomaliza kifungo chake Jumatatu iliyopita Novemba 12, 2018, kwa kusema ilikuwa akipitia kipindi kigumu.

Lulu ametumia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kuelezea hisia zake baada ya kumaliza kifungo cha miaka miwili.

“Kilikuwa kipindi chenye maumivu, matusi, dharau, hukumu za wanadamu, maneno ya kulaaniwa, majina yasiyofaa na mambo mengine mengi ya aina hiyo, lakini namshukuru Mungu yote haya sikuyapokea kama yalivyokuja, bali niliyapokea kama somo/shule iliyojaa utukufu wake,” aliandika Lulu.

==>>Tazama hapo chini alichoandika



from MPEKUZI

Comments