VIDEO: Mwalimu Christopher Mwakasege akieleza Taarifa Ya Kifo Cha mtoto wake

Mwalimu Christopher Mwakasege amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya kifo cha Mtoto wake Joshua ambaye alifariki siku ya Alhamis Saa mbili usiku nakusema katika hali ya kawaida ya kibinadamu asingeweza kuendelea na Semina lakini Mungu alimtia nguvu

“Alhamisi usiku tulifiwa na Mtoto wetu Joshua, alifariki ghafla, halikuwa jambo lepesi kwamba tuendelee na semina au tusiendelee, kwa jinsi ya binadamu halikuwa jambo rahisi kuendelea na semina. Biblia inatuambia tuwe tayari wakati unaofaa na usiofaa

“Haikuwa jambo lepesi kuendelea semina wakati nimefiwa na mtoto wangu Joshua, BIBLIA inasema tuwe tayari wakati unaofaa na usiofaa, Kwa jinsi ya kibinadamu kipindi hiki sio wakati unaofaa kuendelea na semina lakini kwa MUNGU yeye anajua.

“Niliwaomba ndugu zangu niendelee na Semina wakaniuliza una nguvu za kuendelea nikawaambia niombeeni tu! MUNGU atanisaidia” -Mwakasege 

==>>Msikilize hapo chini


from MPEKUZI

Comments