TFF Yatangaza Wajumbe Wapya Kamati Ya Uchaguzi, Nidhamu Na Rufaa Maadili

Kamati ya Utendaji iliyokutana Jumamosi Oktoba 20,2018 Makao Makuu ya TFF Karume, Ilala ilipitia masuala mbalimbali ikiwemo kuchagua wajumbe wa kamati ya Uchaguzi, Kamati ya Nidhamu na Rufaa Maadili.

Pia Kamati ya Utendaji imepitisha tarehe ya Mkutano Mkuu wa TFF wa mwaka. Mkutano huo utafanyika Jijini Arusha Disemba 29,2018

Mkutano huo unafanyika kwa mujibu wa Katiba ya TFF na umepata siku 60 za kutangazwa kabla ya kufanyika

Aidha kikao hicho cha Kamati ya Utendaji kimepitisha mabadiliko madogo kwenye kamati ndogo ndogo za TFF.

Mabadiliko hayo yametokana na baadhi ya Wajumbe kujiuzulu na Wajumbe wengine kukabiliwa na majukumu mengi.

MABADILIKO YA KAMATI ZA  TFF YAPO HAPA CHINI

KAMATI YA UCHAGUZI
1.MALANGWE ALLY -Mwenyekiti
2.Mh . MOHAMED MCHENGELA  -M/Kiti
3.BENJAMINI KARUME   -  Mjumbe
4.MOHAMED GOMBATI  -  Mjumbe
5/HAMISI ZAYUMBA  - Mjumbe

KAMATI YA NIDHAMU
1.KIOMONI  KIBAMBA - Mwenyekiti
2.PETER HELLA - M/Mkiti
3.KASSIM DAU - Mjumbe
4. HANDLEY MATWENGA - Mjumbe
5.  TWAHA MTENGERA - Mjumbe

KAMATI YA RUFAA MAADILI
1.RICHARD MBARUKU - Mwenyekiti
2.THADEUS KARUA  -M/Kiti
3.MH . MUSSA ZUNGU -Mjumbe
4.ASP BENEDICT NYAGABONA-Mjumbe
5.LUGANO HOSEA -Mjumbe


from MPEKUZI

Comments