Ratiba ya Kumuaga mtoto wa Mwalimu Mwakasege

Ratiba ya Kumuaga mtoto  wa Mwalimu Mwakasege  aliyefariki Alhamisi October 11 :- Mwalimu atawasili Dar leo Jumatatu, Jumanne mwili utaagwa Mbezi Beach Lutheran Church, Jumatano alfajiri ni safari kuelekea Mbeya, na Alhamisi ni mazishi Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya

Mahali ulipo msiba; Msiba uko Dar kwa mdogo wake Mwalimu Mwakasege anaitwa Eng. Mwakasingila (Mzee wa kanisa wa KKKT Mbezi Beach)  

Jinsi ya kufika msibani; Fika hadi  Mbezi Beach Jogoo, unaingia barabara ya Karibu Art Gallery kuelekea TAG Mbezi beach kisha utaona vibao vinavyoelekeza msiba ulipo. 

Ratiba ya Jumatatu; Kutakuwa na sala ya pamoja na Mwalimu Mwakasege na familia yeke yote itakayofanyikia hapa msibani itakayoanza saa moja jioni, 7pm itakayoongozwa na Askofu , Mchungaji kiongozi na watumishi wengine  

Kuaga;  Mwili wa marehemu utaagwa Jumanne 16 Oct kanisani KKKT Mbezi Beach Dar, kuanzia saa nane mchana (2pm),  Baada ya kuaga mwili utapelekwa airport kwa ajili ya maandalizi ya safari. 

Kusafirisha: Mwili utasafirishwa Jumatano 17 Oct kwa ndege  

Mazishi:  Yatafanyika alhamisi, Tukuyu, Mbeya 18 Oktoba,2018. 

Muhtasari: Joshua alifariki ghafla baada ya  kudondoka  alhamisi tarehe 11 Oct 2018 akiwa kazini kwake World Bank Dar. Alikimbizwa Aga Khan hospital ila alifariki siku hiyo hiyo.


from MPEKUZI

Comments