Godless Lema Kaitikia Wito wa Jeshi la Polisi

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema leo Jumatatu October 22, ameripoti makao makuu ya Jeshi la Polisi jijini Arusha kama alivyotakiwa kufanya hivyo jana.

Lema amewasili polisi saa 4:55 asubuhi akiwa katika gari aina ya Benzi  na kuegesha gari hilo ndani ya eneo la polisi lakini akatakiwa kuliondoa na kuliegesha nje.

Baada ya kushuka, aliingia polisi akiongozana na Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure, mkewe, Neema na ofisa habari wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Muzeki Joseph.


from MPEKUZI

Comments