Familia ya mfanyabiashara maarufu , Mohammed Dewji ‘Mo’ na Kampuni Tanzu za Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) leo Jumatatu Oktoba 15, 2018 watazungumza na waandishi wa habari kuhusu kutekwa kwa bilionea huyo.
Mkutano huo na waandishi unatarajia kufanyikamchana huu katika ofisi za MeTL zilizopo jengo la Golden Jubilee, Posta jijini Dar es Salaam.
Baba wa ‘Mo’ Gullam Dewji amethibitisha uwepo wa mkutano huo na waandishi wa habari wa vyombo vya ndani na nje ya nchi.
from MPEKUZI
Comments
Post a Comment