BREAKING NEWS: Mo Dewji Kapatikana Akiwa Mzima

Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni ya METL, Mohammed Dewji (MoDewji) amepatikana na kurudi nyumbani kwake salama, saa 9 na dakika 15 Alfajiri hii ya October 20.

Mzee Gulam Hussein amethibitisha mwanaye kupatikana na kurudi nyumbani salama

Pia 'personal Assistant ' (PA) wa Mohammed Dewji Barbara Gonzale amethibitishia  kuwa Mo amepatikana na kuzungumza maneno yafuatayo;

“Namshukuru Mwenyezi Mungu nimerudi salama nyumbani. Nawashukuru Watanzania wenzangu na watu wote kote duniani kwa dua na sala zao. Nashukuru mamlaka zote, ikiwemo Jeshi la Polisi, zilizofanya kazi ya kuhakikisha narudi salama.” — Mohammed Dewji


from MPEKUZI

Comments