Ahukumiwa Miaka 60 Jela Kwa Kumbaka na Kumpa Mimba Mwanafunzi

Mahakama ya Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro imemhukumu kifungo cha miaka 60 jela Abrahamu Kaaya (23) mkazi  wa kijiji cha Karansi wilayani Siha kwa makosa mawili ya kubaka na kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Karansi.

Hukumu hiyo imetolewa leo Jumatatu Oktoba 22, 2018 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Jasmine Abdul baada ya kuridhika na ushahidi wa mashahidi watano.

Mwendesha mashtaka wa Serikali, Simoni Feo amedai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa  alitenda kosa hilo Oktoba 11, 2017 katika kijiji hicho.



from MPEKUZI

Comments